Monday, 24 February 2014

Sehemu Muruwa Kufikia Ukiwa Njombe

Leo nilikuwa Miriam Hotel ambapo nilipokewa na wafanyakazi wake wachangamfu, pichani ni Meneja na Receptionist Tuma.

Mirian Hotel.
Chumbani, baridi ya Njombe sijui itakukutia wapi?



Mgahawa wa Miriam Hotel

Muda wa Lunch umekaribia, wanapatikana kwa namba 0784708811

Monday, 17 February 2014

Vijana wa Njombe

Vijana wa Njombe wakila maisha wikiendi katika moja ya baa za mjini hapa.

Refa Mkongwe Njombe alonga

Huyu ni Zuberi, refa mkongwa sana hapa Njombe. Anasema mpira Njombe umeshuka sana na upinzani wa mpira uliokuwapo siku hizo wakati kuna timu kama Tanwat, Lupembe Chai, Mwenge, Uwemba, Njoss, Kaye (Iliyofungwa 8 na Simba ya Dar es Salaam), Wanging’ombe, Mdandu na Ujenzi zilizokuwa zikichangiwa na wapenzi wa mpira wakiongozwa na Mzee Keneth Mbeyela aliyeleta wachezaji kama Matemo na Juma Misosi kutoka Tanga. Anaikumbuka timu ya Kaye iliyowahi kutoa mchezaji aliyeweza kuchezea timu ya Vijana ya Kanada, Matemo.

Anasema sasa hivi utaalamu umepungua kwani wachezaji wanacheza kiurafiki sana, hata pasi waangaliana sura kwanza ndipo wapasiane.

Pia ujio wa timu kutoka nje ya Njombe umekuwa hadimu sana uliosababisha wachezaji kama Edward Mapunda, Method Mlowezi, Fr. Peter Wella wacheze kwa bidii sana.

Zuberi anashauri ili soka la Njombe lirudi kama zamani inatakiwa Afisa Utamaduni akae na wadau wa zamani waliopo kama Fr. Wella, Abdul wa Tanwat naMzee Kahemele na kuangalia nini kifanyike.Pia mashirika ambayo sasa ni mengi sana hapa Njombe yaangalie uwezekano wa kuanzisha timu na kuleta timu zishindane na timu za Njombe.

Wednesday, 12 February 2014

NG'OMBE WA KISASA UWEMBA


Ng'ombe  wa kisasa wanaofugwa na Watawa Wabenedictini wa Uwemba.

MITAA YA MATALAWE

Hivi Njombe tumeishiwa majina ya Kibena mpaka tukopi na kupesti majina ya Kizaramo?

Monday, 10 February 2014

CHADEMA WASHINDA UDIWANI NJOMBE

Wananchi wa Njombe wakisubiri matokeo.

Wananjombe wakimshangilia Diwani Mteule.

Mh. David Silinde akitangaza matokeo.

Wananjombe wakishangilia matokeo kabla ya kuanza kuzunguka mitaani kushangilia ushindi ambapo walitawanywa na polisi kwa kupigwa mabomu ya machozi.

Friday, 7 February 2014

Mpambano wafikia tamati


Mpambano wa kugombea kiti cha udiwani kata ya Njombe mjini unafikia tamati kesho kutwa kwa wananchi wa Njombe kuamua wanamtaka nani awe diwani wao baada ya kifo cha Jackies.

Mpambano huo uliokuwa wa kukamiana ulijaa vituko na matukio mbalimbali ikiwapo polisi kupigwa na wafuasi wa CCM, wafuasi wa CDM kushitakiwa mahakamani kwa kuwashambulia wana CCM na kumtishia maisha Jah People na vijembe mbalimbali visivyoandikika.

Vyama vyote vinasemekana vimeleta wabunge kutoka sehemu mbalimbali kuongeza nguvu ambapo CDM wamemleta David Silinde wa Mbozi wakati CCM wamewaleta John Nchimbi wa Songea, Deo Sanga, Deo Filikunjombe wa Ludewa, Kayombo wa Mbinga na Pindi Chana naibu Waziri wa Jinsia na Watoto.

Mpambano huo utahitimishwa kwa mikutano mikubwa itakayofanyika Jumamosi sehemu mbalimbali za mji wa Njombe.

Kampeni Njombe

Mbunge wa Mbozi Magharibi Davidi Silinde, akiwa na mgombea udiwani wa kata ya Njombe mjini kupitia CDM wakisalimiana na wananchi kabla ya kuanza mkutano eneo la soko kuu mjini Njombe.

Wednesday, 5 February 2014

Uruhudzi

Mto Ruhuji ukitiririka.

Mitaa ya Nyamuyuya

Sasa hivi nyumba zimefika Mto Ruhuji.

Mitaa ya Nyamuyuya

Mitaa hii zamani kuliitwa Uzunguni Tanesco, siku hizi kunaitwa Nyamuyuya.

African potato

Nimemkuta dada mmoja akichimba mmea huu ambapo anautumia kama dawa. Ameniambia kuwa unatibu magonjwa zaidi ya mia moja.

Thursday, 30 January 2014

Machinjio ya Mabatini

Hapa ni machinjio ya siku nyingi sana hapa Njombe ingawa hivi sasa haitumiki.

Kutiana Umaskini


Wananchi wa Njombe hutegemea sana miti kujenga maisha yao. Tatizo ni moto. Miti yenye umri wa miaka 7 inapoungua halafu mtuhumiwa anatozwa faini ya sh. 20,000 ni jambo la aibu sana.

Wednesday, 29 January 2014

Nyuma ya Airport ya Njombe na kulikokuwa na mshamba ya Magereza




Mto Nyakamtwe

Mto wa Nyikamtwe ukiwa umezungukwa na mashamba.

Ng'ing'i

Mashamba ya numbu hapa Njombe

CDM wakiwa kwenye kampeni za udiwani

Viongozi wa CDM Njombe wakiwa na mkuu wa mafunzo wa CDM kanda ya Nyanda za juu.

Wananchi wakazi wa Ndzengelindete wakisikiliza sera za CDM.

Katibu wa wilaya wa CDM akiamnadi mgombea wa udiwani kata ya Njombe Mjini Bw. Aggrey Mtambo.

Meneja wa kampeni akimtambulisha mgombea Bw. Mtambo.

Mke wa mgombea wa CDM akmwaga sera.

Bwana Mtambo akimwaga sera mitaa ya Ndzenge.

Tuesday, 28 January 2014

MHESHIMIWA ANGUMBWIKE

Kada maarufu wa CCM na Diwani wa kata yangu ya Mjimwema akiwa katika maandalizi ya kampeni za udiwani.

Msikiti

Msikiti wa mtaa wa Kongo, zamani Mtaa wa Dhambi.